Tanzania logo
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara

Mkimbizi ni mtu yeyote ambaye kutokana na hofu ya msingi ya kuteswa kwa sababu za rangi, dini, kabila, uanachama wa kundi la kijamii au maoni ya kisiasa, yuko nje ya nchi yake au nchi ya maskani yake ya kudumu na kwamba hawezi au hayuko tayari kuwa chini ya himaya ya serikali hiyo ambayo ameikimbia.

A refugee is any person whom owing to well-founded fear from persecution for reasons of race, religion, ethnicity, nationality, membership a of particular social group or political opinion is outside his country of nationality or habitual residence and is unable or unwilling to avail himself to the protection of the government which he has previously fled.

Mhamiaji haramu ni raia wa kigeni aliye ndani ya Tanzania na asiye na kibali halali cha kuingia au kuishi Tanzania wakati mkimbizi ni raia wa nchi ya kigeni aliyeomba na kupewa hifadhi kutokana na kuikimbia nchi yake kwa sababu za usalama wake

Illegal immigrant is person who is in Tanzania without the legal right to live or to be in the country while a refugee is a person who has fled from his country for the fear of persecution and has asked asylum and registered in Tanzania.

Waomba hifadhi wote wanapowasili nchini wanatakiwa kuripoti katika Ofisi zozote za Serikali ambako wataelekezwa kufika Idara ya Wakimbizi au kuonana na “Ofisa aliyeidhinishwa” ambaye atawapa utaratibu wa kufuata kufika Ofisi za Idara ambako watahojiwa na kusajiliwa.

All asylum seekers must report to government offices upon their arrival in the country. They will be directed to the Refugee Department or meet with an “authorized officer” who will provide instructions on how to proceed to the department's offices for their interview and registration.

Ifahamike kwamba maeneo wanayoishi wakimbizi ni maeneo tengefu, hivyo wageni wote wanaotaka kuingia katika maeneo haya kwa ajili ya kutoa huduma au sababu zozote zile; watapaswa kuandika barua ya kuomba kibali kwa Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi. Hairuhusiwi kuingia maeneo tengefu bila kibali.

It should be noted that refugees live in designated areas, therefore, Visitors who wish to enter the refugee camps whether to provide services or for any other purpose, must submit a letter to the Director of the Refugee Services Department to request for a camp entry permit. It is strictly prohibited to enter these designated areas without a permit.

Usafirishaji haramu wa binadamu unahusisha kitendo cha kuajiri, kusafirisha, kuficha au kupokea mtu kwa njia ya vitisho, nguvu, udanganyifu au matumizi mabaya ya madaraka kwa lengo la unyonyaji. Unyonyaji unaweza kuwa wa kazi za kulazimishwa, ukahaba, kufanya kazi za ndani, kulazimishwa kuomba mtaani au kushirikishwa katika vitendo vya uhalifu.

Trafficking in persons involves recruitment, transportation, harboring, or receiving of a person by any means including threats, force, deception, or abuse of power for the purpose of exploitation. Exploitation may include forced labor, sexual exploitation, domestic servitude, forced begging, or involvement in criminal activities.

Viini vinavyounda kosa la usafirishaji haramu wa binadamu ni;

·       Tendo Lenyewe: Kusajiri, Kusafirisha, kuhamisha, kuhifadhi, kutoa au kupokea mtu kwa ajili ya kumtumikisha

·       Mbinu: kudanganya, kutisha au kutumia nguvu, kuteka na kutumia mikataba ya uongo

·       Nia/Kusudio: kutumikisha kingono, kufanyisha kazi ngumu, kulazimisha kuomba mitaani, kutoa viungo vya mwili na kufanyisha kazi za ndani

Elements that constitute trafficking in persons offence includes;

  • The act: Recruiting, transporting, transferring, harboring, giving or receiving a person for purpose of exploitation.
  • The means: Use of threats, force, fraud, deception, abuse of power, exploitation of vulnerability, or offering/receiving payments to gain control over a person.
  • The purpose: Exploitation, such as forced labor, sexual exploitation, slavery, organ removal, or other forms of abuse.

Ndiyo. Usafirishaji haramu wa binadamu ni kosa la jinai chini ya Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Sura ya 432. Wahalifu hukabiliwa na adhabu kali ikiwemo kifungo cha maisha gerezani.

Yes, trafficking in persons is a criminal offense under the Anti-Trafficking in Persons Act, Cap. 432. Offenders face heavy penalties including life imprisonment.

Dalili ni pamoja na: haruhusiwi kuondoka sehemu ya kazi, kunyanganywa nyaraka binafsi, kufanya kazi kwa muda mrefu bila malipo au kwa malipo kidogo, anakula mabaki ya chakula kilichoachwa na mwajiri wake, ana makovu au vidonda ambavyo havijatibiwa kutokana na kuteswa, kuonyesha hofu au wasiwasi uliopitiliza, na kutumikishwa kwenye ukahaba au kazi za kinyonyaji.

Restricted movement, lack of access personal documents, working long hours with little or no pay, eat leftovers, has scars or un attended wounds, showing fear or anxiety, being forced into sexual or exploitative work.

Mtu yeyote anaweza kusafirishwa kiharamu, lakini makundi yaliyo hatarini zaidi ni wanawake, watoto, watu wenye ulemavu, maskini na wahamiaji wanaotafuta fursa.

Anyone can be trafficked, but vulnerable groups include women, children, people with disabilities, the poor, and migrants seeking opportunities.

Vichocheo ni pamoja na umaskini, ukosefu wa ajira, mahitaji ya nguvu kazi ya bei nafuu, ukahaba, migogoro ya kifamilia, ukosefu wa elimu, utandawazi, tamaa ya maisha mazuri na faida kubwa wanayoipata wahalifu wanaojihusisha na biashara hii.

Poverty, unemployment, demand for cheap labor, sexual exploitation, family conflicts, lack of education, globalization, dreams of a better life and the profitability of trafficking networks.

Magendo kwa wahamaji yanahusisha kuvuka mipaka kinyume cha sheria kwa ridhaa ya mhusika, na mara nyingi huishia baada ya kuwasili eneo analokwenda. Usafirishaji haramu wa binadamu unahusisha unyonyaji, mara nyingi bila ridhaa, na huendelea hata baada ya kufika mwisho wa safari.

Smuggling is illegal border crossing with consent, usually ending after arrival to the destination. Trafficking involves exploitation, often without consent, and continues even after transportation.

Kwa Waathirika: mateso, msongo wa mawazo, unyanyapaa, magonjwa, kupoteza uhuru na kifo. Kwa Familia: utengano, mzigo wa kifedha. Kwa Taifa: hasara ya kiuchumi, machafuko ya kijamii na kudhalilika kimataifa.

On Victims: abuse, trauma, stigma, diseases, loss of freedom and death. On Families: separation, financial strain. On the Nation: economic loss, social instability, and reputational damage.

Kupitia Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu (Sura 432), kupitia Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Usafirshaji Haramu wa Binadamu, kampeni za uelimishaji, mafunzo na ushirikiano na taasisi mbalimbali zikiwemo za kimataifa.

Through the Anti-Trafficking in Persons Act Cap 432, through Anti-trafficking in Persons Secretariat, awareness campaigns, training, and partnerships with national and international stakeholders.

Ripoti mara moja katika kituo cha polisi, piga simu kwenye namba ya dharura 195 ya Sekretarieti ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, au toa taarifa kwa viongozi wa eneo husika.

Report immediately to the police, call the Anti-Trafficking Secretariat hotline 195, or inform local authorities.

Waathirika hupata msaada wa uokoaji, makazi salama ya muda, huduma za afya, ushauri, msaada wa kisheria, utafutaji wa familia, msaada wa kurejeshwa kwenye jamii, na ulinzi wa haki na utambulisho wao.

Victims receive rescue, shelter, healthcare, counseling, legal aid, family tracing, reintegration support, and protection of identity and rights.

Kujielimisha, kuripoti matukio yanayotiliwa shaka, kusaidia familia zilizo hatarini, na kuelimisha jamii kupitia shule, makanisa, misikiti na mikutano ya kijamii.

Stay informed, report suspicious activities, support vulnerable families, and raise awareness in schools, churches, mosques, and communities.

Tembelea ofisi ya Sekretarieti au tovuti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, fuatilia kampeni za uelimishaji, au piga simu kwa namba ya dharura 195.

Visit the Anti-trafficking in Persons Secretariat office or Ministry of Home Affairs’ website, follow awareness campaigns, or call the national hotline 195.